Matangazo yanakaribishwa katika blog hii,piga simu no 0753 239 687 Email-livinusferuzi@yahoo.com

Tuesday, December 4, 2012

SOKO KUU BUKOBA KUANZA KUJENGWA BAADA YA TARATIBU KUKAMILIKA


 Mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba Khamis Kaputa akitoa ufafanuzi juu ya  miradi ambayo itatekelezwa katika manispaa hiyo ambayo ni pamoja na ujenzi wa soko jipya ,upimaji wa viwanja, ujenzi wa kitega uchumi na standi mpya ya mabasi.
 
Wakuu wa idara mbalimbali za manispaa ya Bukoba waliohudhuria mkutano baina ya  mkurugenzi wa manispaa ya Bukoba na waandishi wa habari
 Baadhi ya waandishi wakifuatilia tamko la mkurugenzi wa manispaa ya Bukoba Khamis Kaputa kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa soko kuu la mjini Bukoba.


 
Na Livinus Feruzi
Bukoba 

HALMASHAURI ya Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera,imesema ujenzi wa soko jipya la kisasa utaanza mara baada ya taratibu kukamilika,huku ikisisitiza kuwa haijafikia hatua ya kutangaza zabuni ya ujenzi wa soko hilo.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba Khamis Kaputa amesema hayo weakati akizungumza na waandishi wa habari kufuatia agizo la kamati ya halmashauri ya kuu ya  Chama cha Mapinduzi mkoani Kagera ambalo liliitaka serikali kutoa taarifa sahihi juu ya miradi yote ya maendeleo inayotarajiwa kujengwa ili kuepukana na kero kutoka kwa wananchi.

Kaputa amesema kuwa upembuzi hakinifu wa mradi wa ujenzi wa ujenzi wa soko jipya,haujawafikisha katika hatua ya kutangaza zabuni na kueleza kuwa iwapo mradi huo utatekelezwa, mapato yatapanda kutoka wastani wa milioni 168 hadi bilioni mbili kwa mwaka.

No comments:

Post a Comment