Matangazo yanakaribishwa katika blog hii,piga simu no 0753 239 687 Email-livinusferuzi@yahoo.com

Friday, December 7, 2012

SUMATRA YAKUTANA NA WADAU WA USAFIRI NA USAFIRISHAJI

Baadhi ya washiriki wa mkutano wa kukusanya maoni juu ya mapendekezo ya kupanda kwa nauli

Baadhi ya wadau wa usafiri na usafirishaji kutoka sehemu mbalimbali za mkoa wa Kagera wakati wa mkutano wa kupokea maoni ya upandishaji wa nauli
 
Kaimu mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo Bw. Ahmad Kilima akizungumza wakati wa mkutano wa kukusanya maoni kuhusu mapendekezo ya viwango vya juu vya nauli za mabasi ya masafa marefu vilivyopendekezwa na wasafirishaji.

Na Mwandishi wetu
Bukoba 
 
Wakitoa maoni juu ya kupanda nauli baadhi ya wadau waliwashutumu  wasafirishaji mkoa wa Kagera kukaidi kufuata nauli zinazopangwa na SUMATRA, ambapo wanajipangia nauli wanazotaka wao, na kuongeza kuwa hakuna ya wao kuomba kupandishiwa nauli kwani tayari walishajipandishia.



Bw. Idrissa Suleiman alisema kigezo wa wasafishaji cha kuomba kupandishiwa nauli kwa sababu ya kupanda kwa gharama za maisha sio sahihi kwani gharama za maisha zimepanda kwa kila mwananchi na sio wasafarishaji tu.

Hata hivyo alitahadharisha kwamba endapo SUMATRA watakubali kupandisha nauli kama walivyopendekeza wasafirishaji gharama za maisha zitazidi kupanda zaidi kwani mahitaji ya msingi ya binadamu yanategemea usafishaji.


No comments:

Post a Comment