Mkuu wa TAKUKURU mkoa
wa Kagera Bi. Domina Mkama aliyekalia kiti kirefu katikati akifuatili michezo mbalimbali wakati wa tamasha hilo.
Na
Mwandishi wetu
Bukoba
WANAFUNZI
wa klabu za wapinga rushwa nchini, wametakiwa kutojiingiza katika vitendo vya
ukiukwaji wa maadili, ikiwemo vitendo vya wizi wa mitihani na rushwa ya ngono.
Kauli
hiyo ilitolewa na afisa uchunguzi wa
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kutoka makao makuu jijini
Dar-es-Salaam, Bw. William Hergard wakati akitoa mada juu ya wajibu wa wanachama wa klabu za wapinga rushwa
katika mapambano dhidi ya rushwa.
Bw.
Hergard aliwataka wanaklabu hao kuwa jasiri kukemea vitendo vya rushwa
vinavyojitokeza ndani na nje ya shule na kufikisha elimu ya rushwa kwa
wanafunzi wenzao ikiwa ni pamoja na jamii inayowazunguka.
MWISHO. |
No comments:
Post a Comment