Matangazo yanakaribishwa katika blog hii,piga simu no 0753 239 687 Email-livinusferuzi@yahoo.com

Saturday, October 13, 2012

KCU KAGERA WAMDANGANYA WAZIRI CHIIZA

waziri wa chakula, kilimo na ushirika Bw. Christopher Chiiza akizungumza na wajumbe wa bodi ya chama kikuu cha ushirika mkoa wa Kagera KCU juu tuhuma za wizi ndani ya chama hicho

Mwenyekiti wa bodi ya KCU bw. John Binushu akisoma taarifa za chama hicho ingawa maelezo yake walikuwa taofauti na hali halisi na hivyo kwa wakulima na watu wengine wanaofahamu KCU

baadhi ya viongozi wa KCU wakimsikiliza waziri CHIIZA

Na mwandishi wetu. Bukoba
WAZIRI wa kilimo chakula na ushirika Bw. Christopher Chiza amewatuhumu wakaguzi wa vyama vya ushirika kuwa chanzo za kudhoofisha ushirika kwa kile alichodai wanapotumwa kufanya ukaguzi wanakuja na taarifa nzuri licha ya kuwepo malalamiko ya matumizi mabaya ya fedha.

Waziri Chiza alitoa kauli hiyo mjini Bukoba wakati akizungumza na wajumbe wa bodi ya chama kikuu cha ushirika mkoa wa Kagera KCU 1990 LTD baada ya malalamiko na tuhuma zilizoibuliwa hivi karibuni juu ya matumizi mabaya ya fedha.

Alisema yanapotokea malalamiko kwenye vyama vya ushirika, wakaguzi wanatumwa kukagua matumizi ili hatua za kisheria na kinidhamu ziweze kwa wahusika lakini wanapokwenda kukagua wanaandaa taarifa nzuri zinaonyesha hakuna matumizi mabaya ya fedha .

“Licha ya kuwepo malalamiko mengi ya KCU kula fedha za wakulima wakaguzi kila wakienda kukagua wanaleta taarifa nzuri na tayari zipo taarifa kwamba wanapotumwa  wanapewa fedha na kuandaa taarifa nzuri ambazo hazionyeshi kasoro” alisema Waziri Chiza.

Kwa mujibu wa waziri Chiza ushirika kwa sasa umedorola taofauti na ilivyokuwa miaka iliyopita na kuwa ofisa yake ina mafaili mengi ambayo yanaonyesha KCU wanakula fedha za wakulima.

Alisema miongoni mwa sababu za kudorola kwa ushirika ni ukosefu wa uaminifu na viongozi wanaochaguliwa kuongoza ushirika huo kupenda kujinufaisha wao badala ya wakulima ambao ndio walengwa na wamiliki wakuu wa ushirika.

Awali akitoa taarifa kwa waziri huyo Mwenyekiti wa bodi ya KCU Bw. John Binunshu alisema kwa sasa KCU haina tatizo kwani wastani wa shilingi milioni 10 hutolewa kila chama kila wiki kwa ajili ya malipo ya wakulim.

Hata hivyo taarifa hiyo ilionekana kupingana na hali halisi ilivyo baada ya kudai kwamba mkoani Kagera hakuna waganda wanaonunua kahawa kwa bei nzuri tofauti na KCU, ambapo kauli hiyo inapingana na kauli ya baadhi ya wakulima wilayani Muleba ambao hivi karibuni walikaririwa wakigoma kuiuzia KCU kahawa baada ya kushusha bei.


Mwisho


No comments:

Post a Comment