Matangazo yanakaribishwa katika blog hii,piga simu no 0753 239 687 Email-livinusferuzi@yahoo.com

Friday, October 5, 2012

BEAKING NEWS:KARDINALI WA KWANZA AFRIKA KUZIKWA KESHO

Mwonekano wa sasa wa kanisa katoliki jimbo la Bukoba, humu ndipo marehemu kardinali Laurean Rugambwa atazika kama makao yake ya milele
-->

Na mwandishi wetu 
Bukoba
BAADA ya maandalizi ya muda mrefu ya kuhamisha masalia ya mwili wa aliyekuwa Kardinali wa kwanza Afrika, marehemu Laurean Rugambwa kutoka katika kanisa la Kashozi alikozikwa kwa muda sasa masalia hayo yataamishwa rasmi kesho, huku Waziri mkuu Bw. Mizengo Pinda akitarajiwa kuwasili kesho mjini Bukoba ili kushiriki tukio hilo.

Kanisa kuu jimbo la katoliki ambalo lilikuwa likikarabatiwa kwa muda mrefu sasa limeshuhudiwa likiwa katika maandalizi ya mwisho, ambapo shamrashara za baadhi ya wakazi mjini Bukoba juu ya tukio hilo zikiwa zimeanza.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kagera na kusainiwa na Bw. Richard Kwitega kwa niaba ya katibu tawala mkoa huo, inaonyesha kuwa Waziri Pinda atawasili saa 9.30 alasiri katika uwanja wa ndege uliopo mjini Bukoba.

Bw. Kwitega alisema mbali na Bw. Pinda kushiriki mazishi ya Kardinali Rugambwa jumapili wiki hii pia atashiriki katika kutabaruku kanisa kuu la jimbo katoliki la Bukoba kabla ya kuondoka mjini Bukoba saa 10 alasiri siku ya jumapili(7/10/2012).

Askofu msaidizi Jimbo katoliki la Bukoba Dkt. Methodius Kilaini alisema sherehe ya kuhamisha masalia ya kardinali Rugambwa kutoka maziko ya muda katika kanisa Kashozi la Mama Bikira Maria, inaambatana na maadhimisho ya miaka 100 tangu kuzaliwa  kwake

-->

No comments:

Post a Comment