Matangazo yanakaribishwa katika blog hii,piga simu no 0753 239 687 Email-livinusferuzi@yahoo.com

Thursday, September 6, 2012

SHIVYAWATA KAGERA WATAKA KUONDOLEWA DOSARI UKUSANYAJI WA MAONI YA KATIBA MPYA

Baadhi ya wajumbe wa tume ya kukusanya maoni ya katiba mpya

Na Mwandishi wetu
Bukoba

SHIRIKISHO la vyama vya watu wenye ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) mkoa wa Kagera limeitaka tume ya mabadiliko ya katiba mpya kurekebisha kasoro zilizojitokeza kwa walemavu wakati wa mikutano ya kutoa maoni juu ya uundwaji wa katiba mpya ili katiba itakayopatika iwe ya Watanzania wote.
 
Kauli ya shirikisho hilo imekuja wiki chache baada ya tume ya mabadiliko ya katiba mpya kuhitimisha zoezi la ukusanyaji wa maoni ya wananchi katika mkoa wa Kagera, ambapo changamoto kubwa ilionekana kuwa ni makundi mengi ya walemavu kushindwa kutoa maoni yao kutokana na kukosa mawasiliano.
 
Mwenyekiti wa SHIVYAWATA mkoa wa Kagera Bw. Suleiman Idrissa alisema hayo leo (jana) mjini Bukoba wakati wa semina ya siku nne kwa watu wenye ulemavu kutoka wilaya ya Muleba na Missenyi juu ya sheria ya ajira ya mwaka 2004 na sheria ya walemavu mwaka 2010 kuhusu mahusiano kazi ni.
 
Bw. Idrissa alisema tathimini iliyofanywa na shirikisho hilo baada ya tume kumaliza zoezi hilo mkoani hapa imebaini kuwa asilimia kubwa ya walemavu hasa wasioona, wasiosikia na viziwi hawakufanikiwa kutoa maoni yao licha ya kujiandaa siku nyingi kwa ajili ya zoezi hilo.
 
Alisema hata baadhi ya walemavu waliofika kwenye mikutano ya kukusanyia walishindwa kufikisha maoni yao kwa tume husika baada ya kukosa mawasiliano baina yao, maandishi wa nukta kwa watu wasioona na watu wa kutafsiri lugha za ishara .
 
 
Hata hivyo shirikisho hilo limesema kwa mapungufu yaliyojitokeza tayari wameingiwa na wasiwasi kama katiba itakayopatikana itakidhi matakwa ya walemavu kutokana kile alichodai kwamba walemavu ndio waathirika wakubwa wa katiba iliyopo.

No comments:

Post a Comment