Matangazo yanakaribishwa katika blog hii,piga simu no 0753 239 687 Email-livinusferuzi@yahoo.com

Wednesday, June 27, 2012

CHUO CHA LAKE ZONE CHAENDELEA KUWANOA MADEREVA KAGERA JUU YA AJALI ZA BARABARANI

Mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani mkoa wa Kagera Bw. Winston Kabantega ambaye pia ni mkurugenzi wa chuo cha mafunzo cha lake zone akiwa na mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Kagera Bw. William Mkonde wakisaini vitabu vya wageni baada ya kuwasili katika kituo cha polisi cha Kamachumu kwa ajili ya kufungua mafunzo ya muda mfupi yanayotolewa kwa madereva.
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Kagera Bw. Winston Kabantega akitoa somo kwa waendesha pikipiki na magari kutoka kata ya Kamachumu wilaya ya Muleba jinsi ya kukabiliana na ajali za barabarai za mara kwa mara

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Kagera Bw. William Mkonde akizungumza na madereva wa magari na pikipiki kutoka kata ya Kamachumu ikiwa ni mara yake ya kwanza kukutana na madereva hao tangu kuhamia mkoa wa Kagera, ambapo alifungua rasmi mafiunzo hayo ya bwiki moja.
Baadhi ya madereva wa magari na pikipiki wakifuatilia maelezo jinsi ya kukabiliana na ajali za barabarani wakati wa mafunzo ya muda mfupi.

Na mwandishi wetu
Muleba
MADEREVA wa magari na pikipiki mkoa wa Kagera wameshauriwa  kuacha tabia ya kuwaona askari wa usalama barabarani kama ‘wanonko’  kutokana na kuwakamata na kuwawajibisha wanaokwenda kinyume na badala yake watambue kwamba wanalenga kuokoa maisha yao.


Mkuu mpya wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Kagera Bw. William Mkonde alitoa wito huo jana katika kata ya Kamachumu wilayani Muleba wakati akifungua mafunzo ya waendesha pikipiki na magari ikiwa ni mara yake ya  kwanza kukutana wadereva tangu alipohamia mkoani hapa.


Bw. Mkonde alisema madereva wengi wanachukulia askari wa kikosi cha usalama barabarani kama ‘wanonko’ kutokana na juhudi za kikosi hicho za kuwakamata na kuwajibishwa hasa kwa kukiuka sheria na kanuni za usalama na kuwa juhudi hizo zinalenga kuokoa maisha yao.


Alisema madhara ya ajali za barabarani ni makubwa na kuongeza kuwa mbali na madereva kuonekana waathirika wakubwa pia jamii  taifa kwa ujumla wanaathirika hasa pale raia wanapoteza maisha au kupata ulemavu wa kudumu.

Naye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Kagera Bw. Winston Kabantega alionya madereva kuancha ya dhana ambayo kwa muda mrefu imejengeka miongoni mwao kwamba wanaweza kupata leseni mpya za kuendeshea vyombo hivyo bila ya vigezo vilivyotangazwa na serikali.

Bw. Kabantega ambaye pia ni Mkurugenzi wa chuo cha mafunzo ya udereva cha lake zone alisema madereva wengi bado wanafikili kwamba wanaweza kulipa fedha bila ya vigezo na kisha kupatiwa leseni, jambo ambalo alisema kwa sasa haliwezekani.

Mafunzo hayo ya muda mfupi yanatolewa na chuo cha Udereva cha lake zone kwa kushirikana na jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani ikiwa ni mwendelezo wa mkakati wa jeshi hilo kutoa elimu kwa madereva mkoani haoa ili kupunguza ajali za mara kwa mara.


Mwisho


No comments:

Post a Comment