Muuguzi mkuu wa mkoa wa Kagera Christine Ntangeki ambaye alikuwa msimamizi wa uchaguzi akitoa wito kwa viongozi hao waliochaguliwa |
Wajumbe wakifuatilia mkutano wa uchaguzi |
Katika ni mwenyekiti wa TANNA tawi la mkoa wa Kagera, ambaye amemaliza muda wake Bw. Deusdedith Rweyemamu akifuatilia matokeo ya uchaguzi yaliyokuwa yakitangazwa na msimamizi wa uchaguzi. |
Safu mpya ya uongozi wa chama cha wauguzi Tanzania tawi la mkoa wa Kagera wakiwa meza kuu baada ya kuchaguliwa wakati wa mkutano mkuu wa uchaguzi. |
Na
Livinus Feruzi
Bukoba
CHAMA
cha wauguzi Tanzania tawi la mkoa wa Kagera kimepata safu mpya ya uongozi baada ya waliokuwepo kumaliza muda wao ambapo Pius
Rugakingira amechaguliwa kuwa Mwenyekiti chama hicho huku Paul Matondane akichaguliwa
msaidizi wake.
Aidha
Evania Fyita alichaguliwa kuwa katibu chama hicho na Gelaid Kabyemela
alichaguliwa kuwa katibu msaidizi, huku Bi. Sofia Musoke ambaye alikuwa Mweka
hazina katika kipindi kilichopita ameendelea kushika nafasi hiyo.
Katika
uchaguzi huo ulifanyika jana muuguzi mkuu wa mkoa wa Kagera Bi. Christine
Ntangeki aliwataka wauguzi mkoa wa Kagera kuhakikisha wanakata leseni za uuguzi
ili waweze kutambuliwa na kukudhi mahitaji ya kisheria ikiwemo kuepukana na
matatizo ambayo wanaweza kukumbana nayo.
Aliwataka
viongozi wa TANNA katika matawi mbalimbali ya mkoa wa Kagera kuwaandikia barua
wauguzi ambao hawana leseni za kuwakumbusha umuhimu na wajibu wao wa kukata
leseni ili waweze kuepukana madhara wanayoweza kukumbana nayo.
Mwisho
No comments:
Post a Comment