Matangazo yanakaribishwa katika blog hii,piga simu no 0753 239 687 Email-livinusferuzi@yahoo.com

Saturday, June 30, 2012

KCU NA MPANGO WA KUUA ZAO LA KAHAWA KAGERA



Baada ya wiki moja blog hii kunukuu wakulima wa kahawa wakigoma kuuza kahawa zao kwa chama kikuu cha ushirika mkao wa Kagera kutokana na kushusha bei ya kahawa gafla tofauti na walivyotangaziwa wakulima wakati wa mkutano.

Barua hii kama inavyoonekana inasema bei ya kahawa aina ya Robusta kwenye soko la dunia ndio imeshuka, huku ikiwa haionyeshi sababu za kupelekea KCU kushusha kahawa aina nyingine ikiwemo Arabica.
Wakulima wanajiuliza maswali ambayo yanakosa majibu kwamba inakuwa Robusta pekee ishuke bei kwenye soko la dania wao KCU washushe kahawa aina nyingine kama sio kutaka kuwakatisha tamaa wakulima wa kahawa? ikumbukwe wanunuzi binafsi bado hawajashusha bei  toa maoni yako ili kusaidia mkulima.

No comments:

Post a Comment