Matangazo yanakaribishwa katika blog hii,piga simu no 0753 239 687 Email-livinusferuzi@yahoo.com

Monday, June 11, 2012

KAGASHEKI ARIDHIA KUVUNJWA KWA SOKO KUU LA BUKOBA

Wananchi wa jimbo la Bukoba wakimpokea mbunge wa jimbo hilo  ambaye pia Waziri wa maliasili na utalii alipowasili katika uwanja wa uhuru kwa ajili ya mkutano wa hadhara
Na Mwandishi wetu 
Bukoba 

WAZIRI wa maliasili na utalii Balozi Khamis Kagasheki ameridhia uamuzi wa kuvunja soko kuu la Bukoba na kulijenga upya ili kulifanya liwe la kisasa huku akiwahakikishia wafanyabiashara katika soko hilo kwamba halitavunjwa mpaka lipatikane eneo mbadala la kufanyia biashara zao.


Balozi Kagasheki ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Bukoba mjini alisema hayo mjini Bukoba katika mkutano wa hadhara, uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye uwanja uhuru, ambapo mkutano huo pamoja na mambo mengine ulilenga kuwashukuru wapiga kura wake.


Alisema suala la kuvunja soko ambalo linapingwa na wafanyabiashara na kisha kupelekea kuwepo kwa mgogoro baina yao na halmashauri ya manispaa ya Bukoba kwa sasa halina nafasi na kusisitiza kuwa lazima livunjwe ili lijengwa upya.


Waziri Kagasheki alisema soko la mjini Bukoba limekuwepo tangu zamani na kuwa miji mingi hapa nchini wamebadili masoko na kujenga  ya kisasa isipokuwa Bukoba na kuongeza kuwa ni lazima hata Bukoba ibadilike ili kwenda na wakati.

MWISHO 

No comments:

Post a Comment