Na Mwandishi wetu
Bukoba
JESHI la polisi mkoa wa Kagera limefanikiwa kukamata bunduki tatu, risasi 246, mabumu matatu ya kurushwa kwa mkono, magazine saba na sare mbili zinazofanana kabisa na za Jeshi la wananchi Tanzania baada ya kudaiwa kumuua mtu mmoja anayesadikiwa kuwa jambazi, wakati wa harakati za kutaka kuvamia mgodi wa Barrick wa Tulawaka uliopo wilayani Biharamulo.
Bukoba
JESHI la polisi mkoa wa Kagera limefanikiwa kukamata bunduki tatu, risasi 246, mabumu matatu ya kurushwa kwa mkono, magazine saba na sare mbili zinazofanana kabisa na za Jeshi la wananchi Tanzania baada ya kudaiwa kumuua mtu mmoja anayesadikiwa kuwa jambazi, wakati wa harakati za kutaka kuvamia mgodi wa Barrick wa Tulawaka uliopo wilayani Biharamulo.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Bw. Philip Kalangi
aliwaambia waandishi wa habari kuwa silaha hizo zilikamatwa mwishoni mwa wiki katika
eneo la Mavota wilaya ya Biharamulo baada ya shambulizi la kurushiana risasi
kati ya askari polisi na mtu anayesadikiwa kuwa jambazi.
Bw. Kalangi alisema polisi walipata taarifa za siri
kutoka kwa raia wema kwamba majambazi wanataka kuvamia mgodi wa dhahabu wa
Tulawaka, ambapo polisi chini ya mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Bw.
Peter Matagi waliweka mtego na hivyo
kufanikiwa kuzima tukio hilo
la ujambazi.
Alitaja aina ya silaha zilizokamatwa kuwa ni pamoja na
bunduki mbili aina ya AK47 na SMG moja, ambapo mbili zilikuwa zimefungwa kwenye
mfuko wa kiroba, huku moja akiitumia kujaribu kujihami, ambayo inaelezwa
haikumsaidia.
Bunduki hizo zilikuwa na
namba UC- 55231990 na UC-16081998 na moja ya SMG yenye namba 56128033262.
Mbali na silahi hizo pia polisi walifanikiwa kukamata
viatu pea moja vya kijeshi na makoti mawili ya kujifuniki mvua, na kuwa mwili
wa jambazi huyo ambaye mpaka sasa bado hajatambuliwa umehifadhiwa katika
hospitali teule ya wilaya Biharamulo.
mwisho
mwisho
No comments:
Post a Comment