Kamanda wa polisi mkoa wa Kagera Bw. Philip Kalangi akionyesha bunduki ambayo ilikamatwa na mfuko wa bangi iliyokamatwa wakati wa operashem maalum pembeni mwake ni mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai mkoa wa Kagera Bw. Peter Matagi.vifaa ambavyo vimekamatwa |
Ni baadhi ya vifaa vya maabara ambavyo vimekamatwa kwa mwalimu Alfred Sitayo akivitumia katika kufundishia masomo ya ziada |
Bukoba
JESHI
la polisi mkoa wa Kagera limefanikiwa kukamata vifaa mbalimbali vinavyosadikiwa
kuwa vya wizi vikiwemo vifaa vya maabara, vitabu, kemikali za maabara ya somo
la kemia ambavyo vinasadikika kuwa mali
ya shule ya sekondari ya Nyakato iliyopo mjini Bukoba.
Kamanda
wa polisi mkoa wa Kagera Bw. Philip Kalangi alisema mwishoni mwa wiki katika
maeneo ya Uganda mwalimu Alfred Sitayo (32)
mkazi wa kata ya Kibeta alikamatwa akiwa na vifaa mbalimbali vya maabara
ambavyo thamani yake bado haijafahamika.
Bw.
Kalangi alisema vifaa hivyo vinasadikiwa kuwa ni mali ya shule ya sekondari ya
Nyakato , ambapo inadaiwa Bw. Alfred Sitayo alikuwa mwalimu katika shule hiyo kwa
upande wa maabara ya kemia kabla ya kuacha kazi.
Alisema
baada ya kuacha kazi mwalimu huyo hakukabidhi maabara ya kemia pamoja na vifaa
vyake katika uongozi wa shule na kuwa alikamatwa na vifaa hivyo akiwa
anavitumia katika kituo chake binafsi ya kufindishia masomo ya ziada tuition.
Aidha
alisema polisi wamekamata vifaa mbalimbali vikiwemo komputa, luninga, radio na
bangi ambavyo vimekamatwa wakati wa operasheni maalum ya jeshi hilo baada ya
kutelekezwa watu wanaosadikiwa kuwa wezi.
mwisho
No comments:
Post a Comment