Frank
Geofray- Jeshi la Polisi, Tabora.
Jeshi la Polisi Mkoani Tabora kwa kushirikiana na
raia wema wamefanikiwa kuwakamata watu watatu wanaotuhumiwa kuhusika na Mauaji
ya Watu wawili ambao ni Mke na Mume tarehe 09 Julai mwaka huu katika Kijiji cha
Inala Kata ya Ndevelwa Manispaa ya Tabora.
Watu hao wanatuhumiwa kuwaua kwa kuwakatakata na
panga Khalid Said (55) na Amina Ally (50) usiku wa siku hiyo wakati walipokuwa
wamepumzika nje ya nyumba yao.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamanda wa Polisi
Mkoani Tabora Kamishna Msaidizi wa Polisi Anthony Rutta aliwataja watuhumiwa
wanaoshikiliwa kuwa ni Mheshimiwa Shakalambe (55) Mkazi wa Naila, Jumanne
Mohamed (30) Msukuma mkazi wa Mbalala Kigwa na Mabula Masanja (33) Msukuma
Mkazi wa Mbuyuni Kigwa.
Kamanda Rutta alisema watu hao walikamatwa katika
msako mkali uliofanywa na Jeshi hilo
mkoani humo ambapo pia wamekutwa na Panga ambalo walilitumia katika kutekeleza
mauaji hayo.
“Watu hawa walitumia mbinu ya kujifanya kuwa ni
wanunuzi wa Ngo’mbe lakini wakati wakiendelea kujadili biashara hiyo walitokea
Vijana wawili ambao kila mmoja wao alikuwa na Panga pamoja na fimbo ndipo
wakatekeleza unyama huo na wamedai kuwa waliahidiwa kulipwa milioni moja au
Ngo’mbe wawili kwa kazi hiyo”
Watuhumiwa hao watafikishwa Mahakamani mara tu baada
ya upelelezi kukamilika na Kamanda Rutta ametoa wito kwa Wananchi kuendelea
kushirikiana na Jeshi la Polisi ili kukomesha Vitendo vya Mauaji na kuwafichua
Wahalifu wa makosa mbalimbali.
|
No comments:
Post a Comment