Matangazo yanakaribishwa katika blog hii,piga simu no 0753 239 687 Email-livinusferuzi@yahoo.com

Tuesday, July 3, 2012

WATUMISHI WANNE WA SERIKALI KAGERA MBARONI KWA RUSHWA

Na Mwandishi maalum
Bukoba.
 
TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa mkoani Kagera (TAKUKURU) inawashikilia watumishi wanne wa serikali kutoka halmashauri ya manispaa ya Bukoba na sekretariti ya mkoa wa Kagera baada ya kutuhumiwa kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu kwa kupitisha mishahara hewa.

Aidha TAKUKURU inaendelea kuwasaka watumishi wengine wanne wa halmashauri ya manispaa ya Bukoba ili waweze kuungana na wenzao katika kujibu tuhuma hizo.

Kaimu kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Kagera Bw. Samsoni Bishati alisema kuwa watumishi hao wanatuhumiwa kupitisha fedha za  mishahara ya watumishi hewa na hivyo kujinufaisha wao wenyewe.

Miongoni mwa wanaoshikiliwa wawili ni kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa huo ambao ni Shabani Kitimbisi na Sifa Musa wote wanatoka idara ya uhasibu na fedha.

Bw. Bishati aliwataja wengine kuwa Davidi Buhenyenge na Martini Muganyizi wote idara ya afya kutoka halmashauri ya manispaa ya Bukoba na kuwa watumishi wengine wanne kutoka halmashauri hiyo bado wanaendelea kutafutwa kuhusika na tuhuma hizo.


Mwisho

No comments:

Post a Comment